Saturday, 4 June 2016

WALIMU WA VETA WAMALIZA MAFUNZO ARIMO

Walimu kutoka vyuo vitano vya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) hivi karibu walikuwa katika chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) kujifunza matumizi ya vifaa vya upimaji. Mafunzo hayo ya wiki mbili yalihudhuriwa na walimu kumi (i.e walimu wawili wawili) kutoka vyuo vya VETA vya Mpanda, Singida, Shinyanga, Tabora na Ulyankulu.

Picha ya pamoja wakati wa kufunga mafunzo. Waliosimama kutoka kushoto ni: Colma Charles (Mkufunzi ARIMO), Leonidas Katabalo (Tabora RVTSC), Benitho Kigava(Mpanda RVTSC), Amani Msigomba (Singida RVTSC), Niyongabo Jotham (Ulyankulu RVTSC), Said A. Kafilameno (Singida RVTSC), Mussa Mashimba (Ulyankulu RVTSC), Salu Mashimo(Shinyanga RVTSC), Tumaini Mzuma (Tabora RVTSC) na Florence Kihundo (Shinyanga RVTSC). Waliokaa kutoka kushoto ni : Cuthbert Kayumbo (Mkufunzi ARIMO), Pius Kafefa (Mkufunzi ARIMO), Eng Daudi Kadinga (Mratibu wa Mafunzo kutoka VETA) na Nkungwe Shomari (Mpanda RVTSC).

Eng Daudi Kadinda akizungumza wakati wa kufunga mafunzo
Baadhi ya washiriki wa mafunzo wakiwa Darasani
Unaweza kupata maelezo mafupi kuhusu mafunzo haya kwa kutazama video iliyopo katika mtando wa Youtube kwa link ifuatayo:

Wednesday, 4 May 2016

MAHAFALI YA 34 YA CHUO CHA ARDHI MOROGORO

Siku ya Ijumaa tarehe 22/4/2016 yalifanyika mahafali ya 34 ya Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO), ambapo wahitimu wa Astashahada ya Awali, Astashahada na Stashahada ya sayansi ya Geomatikia walitunukiwa vyeti. Mgeni wa Heshima katika shughuli hiyo alikuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Angelina S. L. Mabula ambaye aliongozana na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Bwana Yusto Lyamuya. Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Ardhi Morogoro Profesa Mpanduji sambamba na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro Bwana Desderius Kimbe walisisimua sherehe hizo kwa hotuba zao nzuri.

Mheshimiwa Angelina Mabula akiwa na wahitimu wa Chuo cha Ardhi Morogoro

Wanachuo wakisoma risala


Maandamano kuelekea sehemu yalikofanyika mahafali

Mheshimiwa Angelina Mabula

Mwanachuo akitoa maelezo kuhusu matumizi ya DGPS

Wahitimu katika maandamano

Mkurugenzi wa upimaji na ramani Bw. Lyamuya akieleza jambo wakati wa maonesho ya kitaaluma

Mheshimiwa Angelina Mabula akifanya upimaji kwa kutumia darubini

Mheshimiwa Angelina Mabula katika maonesho ya kitaaluma

Mheshimiwa Angelina Mabula akiwa ofisini baada ya kuwasili katika chuo cha Ardhi Morogoro
Mheshimiwa Angelina Mabula alipowasili katika chuo cha Ardhi Morogoro; aliye mbele yake ni Mwenyekiti wa Bodi ya chuo cha Ardhi Morogoro Profesa Mpanduji.

Mkufunzi wa chuo cha Ardhi Morogoro akitoa maelezo kwa Mheshimiwa Angelina Mabula katika maonesho ya kitaaluma